Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Homa ya Findofindo (Tonsillitis)


Utangulizi 

Findofindo ( Tonsillitis) ni nini?

 Mafindofindo ni mashambulizi ya virusi au bakteria kwenye tezi za koo zijulikanazo kama findo. Asilimia 15 mpaka 30 ya mashambulizi haya yanatokana na bakteria ila asilimia kubwa hutokana na virusi. 



Dalili za mafindofindo 

Kwa kawaida ni ngumu kutofautisha kati ya maambukizi yatokanayo na bakteria na yale ya virusi ila leo nitakujuza siri ndogo. Zipo dalili za pamoja na zile za tofauti. 
Zifuatazo ni dalili za pamoja za mafindofindo unazoweza kuzipata kwa wagonjwa waliopata maambukizi ya bakteria na yale virusi 
  • Maumivu ya koo
  • Kupata shida katika kumeza 
  • Homa kali ( Zaidi ya nyuzi joto 38 za sentigredi) 
  • Maumivu ya kichwa
  •  Maumivu ya sikio 
  • Utando katika findo
Dalili zifuatazo zinaasilimia kubwa sana kupatikana kwa mtu mwenye mashambulio yatokanayo na virusi.
  •  Homa ( zaidi ya nyuzi joto 38 za sentigredi) 
  •  Uvimbe shingoni ( upande mmoja au pande mbili) 
  •  Maumivu ya kichwa 
  • Kutokwa na kamasi 
  • Kutokwa na machozi 
  •  Kumeza kwa shida 
  • Maumivu ya koo 
  • Utando mweupe koni 
  •  Kikohozi 
  •  Kupiga chafya

Je ni nini cha kufanya pindi unapokuwa na  dalili hizi? 

Pindi uonapo dalili hizi ni vizuri kufika kituo cha afya kwani kama maambukizi haya yanatokana na bakteria basi utalazimika kutumia dawa malum kwa ajili ya kuua bakteria ( Antibiotics) lakini kama maambukizi yanatokana na virusi basi hutohitajika kutumia dawa hizo na badala yake utashauriwa kutumia dawa za maumivu na kunywa maji mengi kwa siku. 

Ujumbe muhimu

Tambua tofauti za mashambulizi ya virusi na yale ya bakteria ili ukwepe kutumia antibiotics bila sababu.



                                                

                                                    Imetayarishwa na Dr. Umari Ali Jokho,MD.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ualbino (Albinism)

 Ualbino ni nini? Ualbino ( albinism ) ni hali ya kiafya inayotokana na mwili kukosa uwezo wa kutoa homoni aina ya melanin . Homoni hii pamoja na kazi nyingine inahusika na utoaji wa rangi ya mwili. Ukosefu wa melanin huathiri ngozi, macho na nywele.  Ualbino ni hali ya kurithi kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Ikumbukwe kuwa  Albino sio mgonjwa bali ni mlemavu wa macho, nywele na ngozi ambavyo huathiri maisha yake ya kila siku, hata kufupisha umri wa kuishi. Nje na binadamu ualbino unaathiri pia wanyama, samaki, wadudu, nyoka, mijusi, ndege na hata mimea (kwa mimea hutokana na ukosefu wa klorofili).  Waathiriwa wenyewe nchini Tanzania waliamua kupendelea kuitwa "watu wenye ualbino" kutokana na matumizi mabaya ya neno zeruzeru katika utamaduni wa Afrika ya Mashariki ambako watu mara nyingi waliona uhusiano kati ya waathiriwa na mapepo au mizimu. Kuenea kwa Ualbino Tafiti zinaonyesha kuwa mtu mmoja kati ya 20,000 duniani ni albino, lakini kwa sababu zisizofahamika ba...

Maambukizi ya Sikio la Kati (Otitis Media)

  Utangulizi Maambukizi ya Sikio la Kati(Otitis media) ni ugonjwa wa maambukizi yanayoathiri sikio la kati. Sikio la kati ni eneo lililo nyuma ya ngoma ya sikio, ambalo lina nafasi ndogo yenye hewa inayohusiana na sauti. Watoto ndiyo waathirika wakuu wa ugonjwa huu, ingawa watu wazima pia wanaweza kuugua. Maambukizi ya Sikio la Kati inaweza kusababishwa na virusi au bakteria, na mara nyingi huja baada ya kuambukizwa kwa mfumo wa hewa kama mafua au homa. Aina za Maambukizi ya Sikio la Kati Kuna aina kuu tatu za Maambukizi ya Sikio la Kati: Maambukizi ya Sikio la Kati mapya (Acute Otitis Media - AOM) : Hii ni maambukizi ya ghafla kwenye sikio la kati yanayosababisha maumivu makali na dalili kama homa. AOM ni matokeo ya virusi au bakteria, ambapo kioevu hukusanyika kwenye sikio la kati. Maambukizi ya Sikio la Kati yenye usaha (Otitis Media with Effusion - OME) : Hali hii hutokea baada ya AOM ambapo kioevu (liquid)  kinabaki kwenye sikio la kati bila dalili za maambukizi makali. I...

Ugonjwa wa Fistula ( Rectovaginal Fistula)

  Fistula ni nini? Fistula ni tundu lisilo la kawaida linalounganisha sehemu mbili za mwili ambazo kwa kawaida hazipaswi kuungana. Kwa wanawake, hali hii mara nyingi hutokea kati ya  sehemu za siri za mwanamke  na kibofu cha mkojo au njia ya haja kubwa , hivyo kumfanya mgonjwa kushindwa kuzuia haja au kutokwa na haja k ubwa katika  njia ya uzazi .  Mara nyingi husababishwa na kujeruhiwa kwa sehemu hizo wakati wa kujifungua hasa kwa wanawake wanaozaa katika umri mdogo au wanaokosa msaada stahiki wakati wa kuzaa. Kwa mujibu wa shirika la afya duniani,  inakadiriwa kuwa wanawake zaidi ya milioni mbili kutoka Afrika na Asia wanaishi na ugonjwa huu, bila kupatiwa matibabu yoyote, kwa upande wa Tanzania wengi wamekua wakitafuta msaada kwa waganga wa jadi.   Nini Husababisha Fistula? Ugonjwa wa Fistula unaweza kusababishwa na mambo kadhaa ikiwemo yafuatayo; Majeraha wakati wa kujifungua, Maambukizi ya Mfumo wa uzazi (PID), Mgonjwa ya utumbo mpana kama vile Cr...