Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2020

Shinikizo la damu (Hypertension)

Utangulizi Unaweza kuwa na shinikizo la damu (presha) kwa muda mrefu bila kuwa na dalili zozote. Muda wote huu ingawa unakuwa hauna dalili, uwepo wa shinikizo la damu huendelea kuathiri mishipa ya damu na kusababisha madhara makubwa mwilini kama vile magonjwa ya moyo na kiharusi.   Hivyo ni vizuri kujipima mara kwa mara ili kuepuka kuchelewa.     Shinikizo la damu hutokea taratibu kwa kadri umri unavyozidi kuongezeka, hivyo kuathiri karibu kila mtu anapofikia umri mkubwa. Upimaji wake ni rahisi kwa hiyo ni vema ukapima ili kuweza kupambana na ugonjwa huu kwa msaada wa daktari. Dalili Watu wengi wana shinikizo la damu bila kujua au kuwa na dalili. Ni wachahe wanaweza kuwa na dalili kama vile kuumwa kichwa,kutokwa na damu puani na kupata shida ya kupumua. Dalili hizi si maalumu ( spesific) na mara nyingi hazitokei mpaka shinikizo linapokuwa katika kiwango kinachohatarisha maisha. Shinikizo la damu hutokea kwa namna mbili; Kwanza:  Hutokea bila uwepo wa ugonjwa sab

Virusi Vya Korona

Virusi vya Korona ni nini? Virusi vya Corona (Cov) ni familia ya virusi vinavoysababisha ugonjwa kuanzia mafua ya kawaida hadi magonjwa makali zaidi kama vile matatizo ya kupumua (MERS-CoV) na SARS-CoV.  Mwishoni mwa Mwaka 2019,huko nchini China katika mji wa Wuhan kulitokea mlipuko wa  virusi vya korona vilivyopewa jina la COVID-19( Corona virus disease 2019) Baada ya muda mfupi mlipuko huo ulienea sehemu mbalimbali Duniani,hasa katika nchi za Korea ya Kusini, Italya, Iran na Nchi mbalimbali za Ulaya.  Kulingana na maambukizo kusambaa haraka, Shirika la Afya duniani lilitangaza mlipuko huu kuwa wa ngazi ya Pandemia tarehe 30 Januari 2020. Hadi sasa ugonjwa huu umeenea kote Duniani na kusababisha maambukizi kwa zaidi ya   watu 2,320 ,000  vifo zaidi ya watu 160,000 ; huku nchi ya Marekani ikiwa inaongoza kwa idadi   ya wagonjwa wanaozidi laki saba. Ugonjwa wa korona unaambukizwaje? Ugonjwa wa korona unaambukizwa kwa virusi vinavyoachwa hewani kwa