Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Virusi Vya Korona


Virusi vya Korona ni nini?

Virusi vya Corona (Cov) ni familia ya virusi vinavoysababisha ugonjwa kuanzia mafua ya
kawaida hadi magonjwa makali zaidi kama vile matatizo ya kupumua (MERS-CoV) na SARS-CoV. 



Mwishoni mwa Mwaka 2019,huko nchini China katika mji wa Wuhan kulitokea mlipuko wa
 virusi vya korona vilivyopewa jina la COVID-19( Corona virus disease 2019)

Baada ya muda mfupi mlipuko huo ulienea sehemu mbalimbali Duniani,hasa katika nchi za
Korea ya Kusini, Italya, Iran na Nchi mbalimbali za Ulaya. 

Kulingana na maambukizo kusambaa haraka, Shirika la Afya duniani lilitangaza mlipuko
huu kuwa wa ngazi ya Pandemia tarehe 30 Januari 2020.
Hadi sasa ugonjwa huu umeenea kote Duniani na kusababisha maambukizi kwa zaidi ya watu 2,320,000  vifo zaidi ya watu 160,000; huku nchi ya Marekani ikiwa inaongoza kwa idadi ya wagonjwa wanaozidi laki saba.

Ugonjwa wa korona unaambukizwaje?

Ugonjwa wa korona unaambukizwa kwa virusi vinavyoachwa hewani kwa kupiga chafya au kukohoa na kwa njia ya mgusano baina ya watu pale panapokuwa na mgonjwa.
Ukimgusa mtu halafu ukagusa macho,pua, mdomo au kula chakula bila kunawa mikono. 

Kumbuka sio kila mtu mwenye korona anakuwa na dalili,hivyo hasa watu wasio na dalili
ndio wana uwezekano mkubwa wa kusambaza virusi. 

Dalili.

Dalili zake ni pamoja na;
  • Homa,
  • Kikohozi kikavu,
  • Shida katika kupumua, 



na katika hali ngumu zaidi, maambukizi yanaweza kusababisha;
Homa ya mapafu (pneumonia),Kukosa pumzi, Kushindwa kufanya kazi kwa figo na hata kifo.

Jinsi ya Kujikinga.
  • Epuka mkusanyiko wa watu kadri inawezekana, na kama itakulazimu kuwa kwenyemkusanyiko jaribu kuwa katika umbali wa mita 1 au zaidi kati ya mtu na mtu,
  • Nawa mikono kwa sabuni (kwa sekunde 20 au zaidi)  mara kwa mara hasa unapokisha vitu au watu,
  • Epuka kugusa uso mara kwa mara,
  • Acha kuvuta sigara,
  • Tumia vifaa vya kujikinga unapokuwa kwenye mkusanyiko wa watu kama vile maski na gloves.Haishauriwi kutumia vifaa hivi kama upo peke yako,
  • Kaa nyumbani na kujitenga unapohisi dalili hizo hapo juu. 
  • Nenda hospitali kama daili zinazidi.


Kinga na tiba;

Mpaka sasa hakuna kinga,chanjo wala tiba ya virusi vya korona. Juhudi zinafanywa na
mashirika mbalimbali ya afya duniani ili kupata tiba.
Kila nchi ina mfumo wake wa kupambana na Korona. 

Mambo ya kujua kuhusu virusi vya Korona;
  • Kutembea juani,sehemu yenye joto au baridi au kuoga maji ya moto hakuzuii maambukizi,
  • Maambukizi ya korona  yanapona kama magonjwa mengine,kuna uwezekano wa kupata maambukizi mapya baada ya kupona,
  • Kunywa pombe hakuzuii maambukizi,
  • Kuvuta sigara kunachangia maendeleo ya mgonjwa kuwa mabaya,
  • Mbu hawaambukizi korona,
  • Kufunika uso kwa kitambaa hakuzuii maambukizi,
  • Antibiyotik au dawa za malaria haziponyi korona ingawa kuna baadhi ya majaribio ya mchanganyiko wa dawa zinatomia dawa za malaria na virusi.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Msongo wa Mawazo (Depression)

Msongo wa mawazo ni nini? Msongo wa mawazo  ( Depression ) ni mfadhaiko wa akili anaoupata mtu kutokana na shida, taabu, dhiki, matatizo au changamoto zinazomkabili katika maisha ya kila siku. Msongo wa mawazo hutokana na pale mtu anaposhindwa kukabiliana na jambo linalomtatiza. Msongo wa mawazo huwapata watu wa rika na asili zote. Tafiti zinaonyesha kuwa wanawake  hupata msongo wa  mawazo zaidi kuliko wanaume. Msongo wa mawazo ni tatizo la kimwili pamoja na kiakili. Dalili. kujisikia maumivu sehemu mbalimbali za mwili hasa kichwa, kukosa hamu ya kula au kula chakula kupitiliza,hasa vyakula vyenye madhara, kukosa hamu ya tendo la ndoa, kuwa na huzuni wakati wote na kujisikia mnyonge, kusahau kirahisi au kupungua kwa uwezo wa kufikiria, kujisikia mpweke au kukosa matumaini ya maisha, kupungua kwa uwezo wa kimasomo kwa wanafunzi, kuwa na hofu au kutokujiamini, kupungua au kuongezeka uzito bila kupenda, kushindwa kulala au kulala kupindukia, kukosa utulivu wa nafsi, kuba

Homa ya Findofindo (Tonsillitis)

Utangulizi   Findofindo ( Tonsillitis) ni nini?  Mafindofindo ni mashambulizi ya virusi au bakteria kwenye tezi za koo zijulikanazo kama findo. Asilimia 15 mpaka 30 ya mashambulizi haya yanatokana na bakteria ila asilimia kubwa hutokana na virusi.  Dalili za mafindofindo   Kwa kawaida ni ngumu kutofautisha kati ya maambukizi yatokanayo na bakteria na yale ya virusi ila leo nitakujuza siri ndogo. Zipo dalili za pamoja na zile za tofauti.  Zifuatazo ni dalili za pamoja za mafindofindo unazoweza kuzipata kwa wagonjwa waliopata maambukizi ya bakteria na yale virusi  Maumivu ya koo Kupata shida katika kumeza  Homa kali ( Zaidi ya nyuzi joto 38 za sentigredi)  Maumivu ya kichwa  Maumivu ya sikio  Utando katika findo Dalili zifuatazo zinaasilimia kubwa sana kupatikana kwa mtu mwenye mashambulio yatokanayo na virusi.  Homa ( zaidi ya nyuzi joto 38 za sentigredi)   Uvimbe shingoni ( upande mmoja au pande mbili)   Maumivu ya kichwa  Kutokwa na kamasi  Kutokwa na machozi   Kumeza kwa shida  Maum

Shinikizo la damu (Hypertension)

Utangulizi Unaweza kuwa na shinikizo la damu (presha) kwa muda mrefu bila kuwa na dalili zozote. Muda wote huu ingawa unakuwa hauna dalili, uwepo wa shinikizo la damu huendelea kuathiri mishipa ya damu na kusababisha madhara makubwa mwilini kama vile magonjwa ya moyo na kiharusi.   Hivyo ni vizuri kujipima mara kwa mara ili kuepuka kuchelewa.     Shinikizo la damu hutokea taratibu kwa kadri umri unavyozidi kuongezeka, hivyo kuathiri karibu kila mtu anapofikia umri mkubwa. Upimaji wake ni rahisi kwa hiyo ni vema ukapima ili kuweza kupambana na ugonjwa huu kwa msaada wa daktari. Dalili Watu wengi wana shinikizo la damu bila kujua au kuwa na dalili. Ni wachahe wanaweza kuwa na dalili kama vile kuumwa kichwa,kutokwa na damu puani na kupata shida ya kupumua. Dalili hizi si maalumu ( spesific) na mara nyingi hazitokei mpaka shinikizo linapokuwa katika kiwango kinachohatarisha maisha. Shinikizo la damu hutokea kwa namna mbili; Kwanza:  Hutokea bila uwepo wa ugonjwa sab