Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Virusi Vya Korona


Virusi vya Korona ni nini?

Virusi vya Corona (Cov) ni familia ya virusi vinavoysababisha ugonjwa kuanzia mafua ya
kawaida hadi magonjwa makali zaidi kama vile matatizo ya kupumua (MERS-CoV) na SARS-CoV. 



Mwishoni mwa Mwaka 2019,huko nchini China katika mji wa Wuhan kulitokea mlipuko wa
 virusi vya korona vilivyopewa jina la COVID-19( Corona virus disease 2019)

Baada ya muda mfupi mlipuko huo ulienea sehemu mbalimbali Duniani,hasa katika nchi za
Korea ya Kusini, Italya, Iran na Nchi mbalimbali za Ulaya. 

Kulingana na maambukizo kusambaa haraka, Shirika la Afya duniani lilitangaza mlipuko
huu kuwa wa ngazi ya Pandemia tarehe 30 Januari 2020.
Hadi sasa ugonjwa huu umeenea kote Duniani na kusababisha maambukizi kwa zaidi ya watu 2,320,000  vifo zaidi ya watu 160,000; huku nchi ya Marekani ikiwa inaongoza kwa idadi ya wagonjwa wanaozidi laki saba.

Ugonjwa wa korona unaambukizwaje?

Ugonjwa wa korona unaambukizwa kwa virusi vinavyoachwa hewani kwa kupiga chafya au kukohoa na kwa njia ya mgusano baina ya watu pale panapokuwa na mgonjwa.
Ukimgusa mtu halafu ukagusa macho,pua, mdomo au kula chakula bila kunawa mikono. 

Kumbuka sio kila mtu mwenye korona anakuwa na dalili,hivyo hasa watu wasio na dalili
ndio wana uwezekano mkubwa wa kusambaza virusi. 

Dalili.

Dalili zake ni pamoja na;
  • Homa,
  • Kikohozi kikavu,
  • Shida katika kupumua, 



na katika hali ngumu zaidi, maambukizi yanaweza kusababisha;
Homa ya mapafu (pneumonia),Kukosa pumzi, Kushindwa kufanya kazi kwa figo na hata kifo.

Jinsi ya Kujikinga.
  • Epuka mkusanyiko wa watu kadri inawezekana, na kama itakulazimu kuwa kwenyemkusanyiko jaribu kuwa katika umbali wa mita 1 au zaidi kati ya mtu na mtu,
  • Nawa mikono kwa sabuni (kwa sekunde 20 au zaidi)  mara kwa mara hasa unapokisha vitu au watu,
  • Epuka kugusa uso mara kwa mara,
  • Acha kuvuta sigara,
  • Tumia vifaa vya kujikinga unapokuwa kwenye mkusanyiko wa watu kama vile maski na gloves.Haishauriwi kutumia vifaa hivi kama upo peke yako,
  • Kaa nyumbani na kujitenga unapohisi dalili hizo hapo juu. 
  • Nenda hospitali kama daili zinazidi.


Kinga na tiba;

Mpaka sasa hakuna kinga,chanjo wala tiba ya virusi vya korona. Juhudi zinafanywa na
mashirika mbalimbali ya afya duniani ili kupata tiba.
Kila nchi ina mfumo wake wa kupambana na Korona. 

Mambo ya kujua kuhusu virusi vya Korona;
  • Kutembea juani,sehemu yenye joto au baridi au kuoga maji ya moto hakuzuii maambukizi,
  • Maambukizi ya korona  yanapona kama magonjwa mengine,kuna uwezekano wa kupata maambukizi mapya baada ya kupona,
  • Kunywa pombe hakuzuii maambukizi,
  • Kuvuta sigara kunachangia maendeleo ya mgonjwa kuwa mabaya,
  • Mbu hawaambukizi korona,
  • Kufunika uso kwa kitambaa hakuzuii maambukizi,
  • Antibiyotik au dawa za malaria haziponyi korona ingawa kuna baadhi ya majaribio ya mchanganyiko wa dawa zinatomia dawa za malaria na virusi.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ualbino (Albinism)

 Ualbino ni nini? Ualbino ( albinism ) ni hali ya kiafya inayotokana na mwili kukosa uwezo wa kutoa homoni aina ya melanin . Homoni hii pamoja na kazi nyingine inahusika na utoaji wa rangi ya mwili. Ukosefu wa melanin huathiri ngozi, macho na nywele.  Ualbino ni hali ya kurithi kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Ikumbukwe kuwa  Albino sio mgonjwa bali ni mlemavu wa macho, nywele na ngozi ambavyo huathiri maisha yake ya kila siku, hata kufupisha umri wa kuishi. Nje na binadamu ualbino unaathiri pia wanyama, samaki, wadudu, nyoka, mijusi, ndege na hata mimea (kwa mimea hutokana na ukosefu wa klorofili).  Waathiriwa wenyewe nchini Tanzania waliamua kupendelea kuitwa "watu wenye ualbino" kutokana na matumizi mabaya ya neno zeruzeru katika utamaduni wa Afrika ya Mashariki ambako watu mara nyingi waliona uhusiano kati ya waathiriwa na mapepo au mizimu. Kuenea kwa Ualbino Tafiti zinaonyesha kuwa mtu mmoja kati ya 20,000 duniani ni albino, lakini kwa sababu zisizofahamika ba...

Mawe ya Figo (Kidney Stones)

Utangulizi Mawe ya figo ni moja ya matatizo ya kawaida yanayoathiri mfumo wa mkojo. Mawe haya huundwa kutokana na madini na chumvi zinazokusanyika kwenye figo na kuunda uvimbe mgumu kama jiwe. Mawe ya figo yanaweza kuwa madogo kama mchanga au makubwa kiasi cha kuziba njia ya mkojo. Ugonjwa huu unaweza kusababisha maumivu makali sana, hasa mawe yanapohamia kutoka kwenye figo hadi kwenye kibofu au njia ya mkojo (ureter). Aina za Mawe ya Figo Kuna aina nne kuu za mawe ya figo, ambayo hutegemea muundo wa kemikali: Mawe ya calcium oxalate: Haya ndiyo aina ya kawaida zaidi ya mawe ya figo. Hupatikana wakati kuna kiwango kikubwa cha kalsiamu na oxalate kwenye mkojo. Mawe ya uric acid: Haya hutokea wakati mkojo unakuwa na kiwango kikubwa cha asidi. Mara nyingi yanaathiri watu wanaokula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha  nyama nyekundu au wale wenye historia ya ugonjwa wa jongo (gout). Mawe ya struvite: Mawe haya yanaonekana zaidi kwa wanawake na hutokea baada ya maambukizi ya njia ya m...

Maambukizi ya Sikio la Kati (Otitis Media)

  Utangulizi Maambukizi ya Sikio la Kati(Otitis media) ni ugonjwa wa maambukizi yanayoathiri sikio la kati. Sikio la kati ni eneo lililo nyuma ya ngoma ya sikio, ambalo lina nafasi ndogo yenye hewa inayohusiana na sauti. Watoto ndiyo waathirika wakuu wa ugonjwa huu, ingawa watu wazima pia wanaweza kuugua. Maambukizi ya Sikio la Kati inaweza kusababishwa na virusi au bakteria, na mara nyingi huja baada ya kuambukizwa kwa mfumo wa hewa kama mafua au homa. Aina za Maambukizi ya Sikio la Kati Kuna aina kuu tatu za Maambukizi ya Sikio la Kati: Maambukizi ya Sikio la Kati mapya (Acute Otitis Media - AOM) : Hii ni maambukizi ya ghafla kwenye sikio la kati yanayosababisha maumivu makali na dalili kama homa. AOM ni matokeo ya virusi au bakteria, ambapo kioevu hukusanyika kwenye sikio la kati. Maambukizi ya Sikio la Kati yenye usaha (Otitis Media with Effusion - OME) : Hali hii hutokea baada ya AOM ambapo kioevu (liquid)  kinabaki kwenye sikio la kati bila dalili za maambukizi makali. I...