Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers)


Ni vidonda vinavyotokea kwenye ukuta wa ndani wa tumbo au utumbo mwembamba.  Hutokana na tindikali(stomach acids) zinazotolewa na tumbo kusaidia mmeng'enyo wa chakula kuzidi hivyo kuharibu ukuta wa tumbo au utumbo mwembamba. 




Watu wengi wanaweza kuwa vidonda vya tumbo bila kuwa na dalili zozote. Lakini wakati mwingine vidonda vinaweza kutoka damu hadi kuhatarisha maisha kama hatua za dharura hazitachukuliwa.



Sababu

  • Sababu kubwa ya vidonda vya tumbo ni maambukizi ya bakteria anayefahamika kwa jina  la Helicobacter pylori(H. pylori). 
  • Matumizi ya dawa za maumivu kama vile ibuprofen(advil,ibucold, motrin IB n.k), aspirin, na naproxen  kwa muda mrefu.
  • Pombe na sigara.


Msongo wa mawazo na matumizi ya viungo vya chakula havisababishi vidonda vya tumbo lakini vinazidisha dalili za maumivu kwa mtu ambaye tayari ana vidonda.


Dalili




  • Maumivu ya tumbo sehemu iliyopo  kati ya kitovu na kifua, hasa wakati wa njaa kama vile usiku au kati ya mlo mmoja hadi mwingine. Maumivu hupungua baada ya kula au kutumia dawa za anti-asidi lakini baada ya muda huanza tena,
  • Kichefuchefu,
  • Kukosa hamu ya kula,
  • Kucheua mara kwa mara au kupatwa na kiungulia,
  • Kushindwa kula vyakula vya mafuta,
  • Kutapika damu au kupata choo chenye damu au rangi nyeusi,
  • Kujisikia unyonge au kuzimia,
  • Mwili kupungua uzito bila sababu.
Una hatari zaidi ya kupata vidonda vya tumbo kama una haya yafuatayo:
  • Una umri wa miaka 65 au zaidi,
  • Una maambukizi ya vimelea vya H. pylori,
  • Unatumia dawa za maumivu zaidi ya aina moja,
  • Ulishawahi kupata vidonda vya tumbo kabla,
  • Unatumia dawa za steroid.

Pindi utapata dalili mojawapo au kadhaa kati ya hizo hapo juu, daktari atakuuliza kama umetumia kwa muda mrefu dawa za maumivu. Majibu yako yanaweza kutosha kuanzisha matibabu ya anti-asidi na dawa za kupunguza utoaji wa tindikali (PPI). 

Daktari hulazimika kufanya vipimo vya ziada kama dalili zimezidi au mgonjwa ana hali mbaya. Vipimo hivyo ni kama vile pumzi, kupima haja kubwa kwa ajili ya vimelea vya H. pylori. Wakati mwingine kipimo cha kamera tumboni (Endoscopy) hutumika kwa ajili ya  kuchukua sampuli ili kuangalia kama kuna vimelea na kutambua pia ukubwa wa vidonda pamoja na kupambana na tatizo la kutokwa na damu.
 

Tiba

Ili kupunguza uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo wakati unatumia dawa za maumivu;
  • Tumia dozi ndogo kabisa ili kudhibiti dalili na uache kuzitumia mara tu unapokuwa huzihitaji tena,
  • Tumia ukiwa umeshiba,
  • Usinywe pombe au kuvuta sigara wakati unatumia dawa za maumivu,
  • Tumia dawa za kupunguza tindikali kama vile Omeprazole, Pantoprazole n.k, pamoja na anti-acids,
  • Kunywa maji safi na salama,
  • Nawa mikono wakati wa kula,
  • Jifunze kupambana na msongo wa mawazo,
  • Punguza viungo vya chakula unapokuwa na maumivu ya tumbo.
Daktari atakuandikia antibiotics ili kupambana na vimelea vya H. pylori kama vitaonekana kwenye vipimo. Aina za antibiotics na dozi  zipo nje ya makala hii. 







 Ikumbukwe kuwa watu wawili kati ya watatu dunia wana maambuki ya H. pylori lakini wengi hawana vidonda vya tumbo. 




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ualbino (Albinism)

 Ualbino ni nini? Ualbino ( albinism ) ni hali ya kiafya inayotokana na mwili kukosa uwezo wa kutoa homoni aina ya melanin . Homoni hii pamoja na kazi nyingine inahusika na utoaji wa rangi ya mwili. Ukosefu wa melanin huathiri ngozi, macho na nywele.  Ualbino ni hali ya kurithi kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Ikumbukwe kuwa  Albino sio mgonjwa bali ni mlemavu wa macho, nywele na ngozi ambavyo huathiri maisha yake ya kila siku, hata kufupisha umri wa kuishi. Nje na binadamu ualbino unaathiri pia wanyama, samaki, wadudu, nyoka, mijusi, ndege na hata mimea (kwa mimea hutokana na ukosefu wa klorofili).  Waathiriwa wenyewe nchini Tanzania waliamua kupendelea kuitwa "watu wenye ualbino" kutokana na matumizi mabaya ya neno zeruzeru katika utamaduni wa Afrika ya Mashariki ambako watu mara nyingi waliona uhusiano kati ya waathiriwa na mapepo au mizimu. Kuenea kwa Ualbino Tafiti zinaonyesha kuwa mtu mmoja kati ya 20,000 duniani ni albino, lakini kwa sababu zisizofahamika ba...

Mawe ya Figo (Kidney Stones)

Utangulizi Mawe ya figo ni moja ya matatizo ya kawaida yanayoathiri mfumo wa mkojo. Mawe haya huundwa kutokana na madini na chumvi zinazokusanyika kwenye figo na kuunda uvimbe mgumu kama jiwe. Mawe ya figo yanaweza kuwa madogo kama mchanga au makubwa kiasi cha kuziba njia ya mkojo. Ugonjwa huu unaweza kusababisha maumivu makali sana, hasa mawe yanapohamia kutoka kwenye figo hadi kwenye kibofu au njia ya mkojo (ureter). Aina za Mawe ya Figo Kuna aina nne kuu za mawe ya figo, ambayo hutegemea muundo wa kemikali: Mawe ya calcium oxalate: Haya ndiyo aina ya kawaida zaidi ya mawe ya figo. Hupatikana wakati kuna kiwango kikubwa cha kalsiamu na oxalate kwenye mkojo. Mawe ya uric acid: Haya hutokea wakati mkojo unakuwa na kiwango kikubwa cha asidi. Mara nyingi yanaathiri watu wanaokula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha  nyama nyekundu au wale wenye historia ya ugonjwa wa jongo (gout). Mawe ya struvite: Mawe haya yanaonekana zaidi kwa wanawake na hutokea baada ya maambukizi ya njia ya m...

Maambukizi ya Sikio la Kati (Otitis Media)

  Utangulizi Maambukizi ya Sikio la Kati(Otitis media) ni ugonjwa wa maambukizi yanayoathiri sikio la kati. Sikio la kati ni eneo lililo nyuma ya ngoma ya sikio, ambalo lina nafasi ndogo yenye hewa inayohusiana na sauti. Watoto ndiyo waathirika wakuu wa ugonjwa huu, ingawa watu wazima pia wanaweza kuugua. Maambukizi ya Sikio la Kati inaweza kusababishwa na virusi au bakteria, na mara nyingi huja baada ya kuambukizwa kwa mfumo wa hewa kama mafua au homa. Aina za Maambukizi ya Sikio la Kati Kuna aina kuu tatu za Maambukizi ya Sikio la Kati: Maambukizi ya Sikio la Kati mapya (Acute Otitis Media - AOM) : Hii ni maambukizi ya ghafla kwenye sikio la kati yanayosababisha maumivu makali na dalili kama homa. AOM ni matokeo ya virusi au bakteria, ambapo kioevu hukusanyika kwenye sikio la kati. Maambukizi ya Sikio la Kati yenye usaha (Otitis Media with Effusion - OME) : Hali hii hutokea baada ya AOM ambapo kioevu (liquid)  kinabaki kwenye sikio la kati bila dalili za maambukizi makali. I...